Wasichana nchini wameshauliwa kujiunga na vyuo vya elimu na mafunzo ya ufundi stadi ili waweze kushiriki kikamilifu katika kipindi hiki ambacho serikali ina mwelekeo wa kuwa nchi ya uchumi wa viwanda.
Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Mjumbe wa Bodi ya VETA kanda ya Mashariki Beda Marwa wakati wa Mahafali ya 29 ya Chuo cha Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi(VETA) Kihonda Manispaa ya Morogoro baada ya kushuhudia idadi ndogo ya wahitimu wa kike katika mahafali hayo.
“Jamii inatakiwa kuwahamasisha watoto wa kike kusoma mafunzo ya ufundi stadi kwani sera ya uchumi wa viwanda inahitaji watalamu wengi hivyo juhudi zinahitajika kuwahamasisha watoto hawa kwa manufaa ya taifa,”alisema.
Katika mafahali hao wahitimu walikuwa 297 kati yao wavulana walikuwa ni 248 huku wasichana wakiwa 49 tu jambo ambalo lilionekana kumsikitisha Marwa ambapo alisema jitihada zaidi zinahitajika ili uwiano uwe sawa kwa wote.
Aidha Marwa alitawaka wahitimu wote kuwa waaminifu na waadilifu wapatapo kazi, pamoja na kuweka malengo mazuri ya kiuchumi kwa kuanzisha viwanda vidogovidogo pamoja na kukemea vitendo viovu katika jamii.
Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa chuo hicho Maganga Kashindye aliiomba serikali kuwasaidia kutatua changamoto ya uhaba wa mabweni kwani yaliyopo hayajitoshelezi hivyo baadhi ya wanafunzi hulazimika kukaa nje ya chuo na kusababisha usumbufu kwa wanafunzi wanaotoka nje ya mkoa.
Nao wahitimu wa chuo hicho waliomba kuwawezeshwa kupata mikopo itakayowafanya kujiendeleza kiuchimi ikiwa ni pamoja na kuanzisha viwanda hali itakayosaidia kutoa ajira kwa vijana wenzao waliokosa ajira.
VETA HEAD OFFICE,
12 VETA Road.
41104 Tambukareli,
P.O. BOX 802, Dodoma Tanzania,
Email: info@veta.go.tz
Telephone: +255 26 2963661
Fax: +255 22 2863408
Url: www.veta.go.tz
© 2018 - VETA Head Office